Hawa ndio viongozi wapya wa UKWATA MKOA WA IRINGA.
CCT TANZANIA
Maudhui ya kidini na kifalsafa
Jumanne, 17 Juni 2014
Tusisubiri kesho kufanya yale tunayopaswa kufanya.Tufanye SASA, LEO si Baadae wala KESHO
Yapo mambo mengi sana tunayopaswa kujifunza kwayo. Mojawapo ni pale mmoja kati ya watu tuliokuwa tumezoeana nao,tulioishi nao,tuliofurahi nao,hata wale tuliokuwa maadui wanapotutoka na kwenda mahala ambapo hatuwezi kuwa na mawasiliano nao tena katika mwili huu wa nyama. Hebu jiulize ni maneno yapi yatasemwa na watu kuhusu wewe wakiimaanisha utakapokuwa umeondoka ? tafakari kidogo. Je, watakukumbuka kwa mengi mazuri au watakupa sifa bubu zisizo na uhai katika dunia hii ?.
Ndugu zangu Mungu ametupa akili tuzitumie ipasavyo SASA,LEO na si baadae au kesho.Tufanye hivyo kwa mazuri tena bila kuchelea maana hatujui siku wala saa.
Ndugu, rafiki, tungeanza wote mtihani wa kuhitimu Chuo kikuu june/2014, Lakini haiko hivyo tena. Utakumbukwa daima.Amen
Wana CCT RUCO na familia ya wana RUCO pamoja na familia ya marehemu, wakiomboleza
msiba wa mwanajumuia mwenzao Ndugu SUBILI
KILASI aliyekuwa mwanachuo kitivo cha sanaa na sayansi ya jamii aliyefariki siku ya
ijumaa ya tarehe 8/11/2013. Katika utumishi wa kanisa, marehemu Kilasi
alikuwa Mwenyekiti wa Kamati ya chakula na Mwanakwaya wa kwaya ya HOPE akimsaidia m/kit wa nidhamu katika kwaya ya HOPE na aliyemtumikia Mungu kwa nguvu zake zote kwa njia ya uimbaji mpaka mauti
yanamkuta. Hakika ni pengo kubwa lakini katika Kristo tunayo imani kuwa Mungu
aliifurahia kazi yake aliyoifanya kuwahubiri watu kwa njia ya uimbaji.
Jeneza lenye mwili wa marehemu Kilasi ukiwa
nyumbani kwao
Waombolezaji wakiwa wamebeba mwili
wa marehemu kuelekea kwenye nyumba yake ya milele
Safari
ya mwisho ya kumpeleka marehemu kilasi kuelekea kwenye nyumba yake ya milele
Wana
CCT pamoja na wanachuo katika safari ya kulekea makaburiniMwinjilisti akiongoza safari ya kuelekea makaburini kumsindikiza ndugu Kilasi kwenye makazi yake ya milele
Mama mzazi wa marehemu na Waombolezaji wakiweka mashada ya
maua kwenye kaburi la marehemu Kilasi
Jumapili, 4 Mei 2014
CCT Ruaha University College: WANA CCT WAPATA VIONGOZI WAPYA WAPYA WA CCT 2014/...
CCT Ruaha University College:
WANA CCT WAPATA VIONGOZI WAPYA WAPYA WA CCT 2014/...: WANA CCT WAPATA VIONGOZI WAPYA WAPYA WA CCT 2014/2015 Wana CCT wamepata viongozi wapya baada ya uchaguzi uliofanywa na wana CCT kufu...
WANA CCT WAPATA VIONGOZI WAPYA WAPYA WA CCT 2014/...: WANA CCT WAPATA VIONGOZI WAPYA WAPYA WA CCT 2014/2015 Wana CCT wamepata viongozi wapya baada ya uchaguzi uliofanywa na wana CCT kufu...
Ijumaa, 4 Aprili 2014
ALBUM YA KWANZA HOPE CHOIR
Hii ni album yao ya kwanza iitwayo MAISHA,ambayo imekuwa ikishika kasi katika mkoa huu wa Iringa.
Kasha la mkanda wa video wa Hope Choir CCT RUCO
Kasha la mkanda wa Audio wa Hope Choir CCT RUCO
Hope choir wakijifua kwa ajili ya pasaka
Baadhi ya wanakwaya ya Hope (CCT-RUCO) wakiendelea na mazoezi kwa ajili ya sherehe za pasaka na mikesha ya joint fellowship mkoani Iringa.
Kikundi hiki kimekuwa kikifanya vizuri katika tasnia ya uimbaji katika mkoa huu wa Iringa na hivyo kukiwezesha kupata mialiko mbalimbali yakiwemo matamasha,mikutano,sherehe za harusi,na shughuli zingine.
Mwalimu wa kwaya Imani S.Nkolela (shati nyeupe) akiwaelekeza na kuwafundisha wanakwaya.kulia kwake ni m/kiti Laurence Mwamakula akiseti mziki kwenye laptop na katikati ni mdau wa Hope choir Jofrey.
Kwa mbali ni Batungulu Yona akifurahi na kushoto kushoto ni Ibrahim Issa
Kikundi hiki kimekuwa kikifanya vizuri katika tasnia ya uimbaji katika mkoa huu wa Iringa na hivyo kukiwezesha kupata mialiko mbalimbali yakiwemo matamasha,mikutano,sherehe za harusi,na shughuli zingine.
Mwalimu wa kwaya Imani S.Nkolela (shati nyeupe) akiwaelekeza na kuwafundisha wanakwaya.kulia kwake ni m/kiti Laurence Mwamakula akiseti mziki kwenye laptop na katikati ni mdau wa Hope choir Jofrey.
Kwa mbali ni Batungulu Yona akifurahi na kushoto kushoto ni Ibrahim Issa
Jisajili kwenye:
Machapisho (Atom)